Msajili wa baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania anapenda kuwatangazia Wananchi  wote  kuwa  Baraza  la  Uuguzi  na Ukunga  Tanzania  linatimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwake.

Kuelekea Sherehe za Maadhimisho hayo kutakuwa na maonyesho na huduma mbalimbali za Kiuuguzi zitakazotolewa kuanzia tarehe  17/3/2023 hadi   tarehe  19/3/2023   katika   viwanja   vya   Nyerere   square   Jijini Dodoma.

File Type: pdf