THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania limeendesha Mafunzo ya namna ya kushiriki utoaji huduma katika chumba cha upasuaji kwa Wauguzi na Wakunga katika Hospitali ya St. Benedict iliyopo Ndanda – Halmashauri ya Masasi,Mkoani Mtwara ambapo washiriki walikuwa ni Wauguzi na Wakunga, wataalamu wa dawa za usingizi na ganzi pamoja na Madaktari wa upasuaji. 

Akitoa mafunzo hayo Afisa Muuguzi Mbobezi Kitengo Cha Upasuaji Bi. Salome Kassanga amewataka watumishi yale waliyoyapata kutoka katika mafunzo hayo ili kuhakikisha jamii inapata huduma iliyo bora na salama.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dr. Isaiah Michael Sienz amesema mafunzo hayo yamesaidia kuboresha mazingira ya vyumba vya upasuaji na kuwaongezea ujuzi watumishi hao ambapo hapo awali hawakuwa na ujuzi huo kutokana na kutosoma namna ya kutoa huduma ya aina hiyo, baada ya mafunzo kusitishwa hapa nchini.

Pamoja na mafunzo hayo Dr.Sienz amemshukuru Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania Bi.Agnes Mtawa kwa jitihada za utoaji wa mafunzo ya aina hiyo kwa watumishi waliopo kazini huku akiiomba serikali irudishe mafunzo hayo ili kuboresha utoaji wa huduma ya aina hiyo kwa wateja mbalimbali.

Mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na wauguzi na wakunga zaidi ya 40 pamoja na wauguzi watarajali yanatarajiwa kuwa chachu ya utoaji wa huduma bora Mkoani Mtwara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *