THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania limendelea kuwajengea uwezo Wauguzi na Wakunga nchini kwa kuwafundisha jinsi ya kutoa huduma wanaposhiriki zoezi la upasuaji katika chumba cha upasuaji ili kuboresha huduma na mara hii, mafunzo hayo yamefanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Ligula Mkoani Mtwara.

 Mafunzo hayo yanayowahusisha Madaktari, Wauguzi na Wakunga pamoja na wahudumu wa Afya wapatao 45 kutoka chumba cha upasuaji, chumba cha wagonjwa wanaohitaji ungalizi karibu, idara ya kusafisha na kutakasa vifaa tiba, sehemu ya huduma za dharura, wodi ya Wazazi sanjari na wodi ya upasuaji.

Akifafanua juu ya umuhimu wa mafunzo hayo Bi. Salome Kasanga, ambaye ni Muuguzi mtaalamu wa chumba cha upasauaji kutoka Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania amesema, mafunzo hayo yanafanyika chini ya uratibu wa Baraza kwa siku 14 yakiwa na alama 11.4 za mafunzo ya kujiendeleza kazini yakitumia moduli 06 katika usimamizi wa chumba cha upasuaji.

“Kumekuwa na changamoto ambapo baadhi ya watumishi hawana ujuzi wa kutosha wa kusimamia na kuendesha huduma katika vyumba vya upasuaji hivyo nia ya mafunzo haya ni kuwajengea uwezo ili kuzuia maambukizi kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji”

Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania likiwa ni sehemu ya Taasisi za Wizara ya Afya, lilianzishwa mwaka 1953 ili kusimamia taaluma ya Uuguzi na Ukunga Nchini likiahakikisha kuwa wataalaumu wa kada hizo wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi na maadili ya taaluma hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *