THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Wanafunzi wanaosoma taaluma ya Uuguzi na Ukunga katika Vyuo mbalimbali Nchini, wameshauriwa kuzingatia mafunzo kwa vitendo wanapokuwa vyuoni ili kuwa na umahiri unaotakiwa katika taaluma ya Uuguzi na Ukunga pamoja na kufaulu mitihani ya usajili na leseni inayoratibiwa na Baraza.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa mafunzo na maendeleo ya taaluma wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania Bi. Happy Masenga, alipozungumza na kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa umma cha Baraza la Uuguzi na Ukunga Jijini Dodoma.

“Kwa kusema hayo, basi niweze pia kuwashauri wanafumnzi waliopo vyuoni wanaosoma taaluma ya Uuguzi na Ukunga kwamba, wanapokuwa katika mafunzo wazingatie sana kujifunza kwa vitendo katika Hospitali wanazotakiwa kujifunza kwa vitendo, hii inamsaidia sana kuwa na kumbukumbu katika mitihani ya usajili na leseni lakini pia kujenga umahili unaotakiwa”

Akizungumzia kuhusu vyuo vya uuguzi na Ukunga vilivyosajiliwa kuendesha mafunzo nchini, Mkurugenzi Bi.Masenga, amevitaka Vyuo hivyo kuendesha mafunzo kwa kuzingatia mitaala sanjari na kuwafuatilia wanafunzi wao wanapokuwa katika maeneo ya kujifunza kwa vitendo ili kutoa wauguzi wenye ubora na umahili unaotakiwa.

Katika hatua nyingine Bi.Masenga, amebainisha awamu tatu za kufanyika kwa mitihani ya leseni kuwa ni Mwezi wa 12, 04, 08 au mwezi wa tisa kwa  kila mwaka wa Fedha wa serikali pia amewataka wahitimu wanaoomba kusajiliwa kufanya mtihani  wa usajili na leseni hususani unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao, kuchagua vituo vilivyo karibu na Mikoa wanayoishi na kubainisha vituo saba kuwa ni Pamoja na Taasisi ya Afya na Sayansi Shirikishi Tandabui Mwanza, Chuo Kikuu cha Kampala Dar es Salamu, Chuo cha St. John Dodoma, Chuo cha Stephano Moshi- Kilimanjalo, Chuo cha Afya na Sayansi shiriki – Mbalizi Chuo Kikuu cha Katoliki Iringa (RUCU) Pamoja na  Tabora Polytechnic Mkoani Tabora.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *