THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Maadili,Usajili na Leseni Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania Bi.Jane Mazigo wakati wa mafunzo na sheria ya uuguzi na ukunga yaliyofanyika Halmashauri ya Kibaha katika ofisi za baraza la uuguzi na ukunga mkoani Pwani.

kwa upande wake Mwanasheria wa baraza la uuguzi na ukunga Tanzania Isaya Nkya wakati wa mafunzo hayo ya sheria na maadili kwa Wauguzi na Wakunga amewataka wauguzi na wakunga wote nchini kuacha tabia ya kumtelekeza mteja kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Ikumbukwe kuwa Wauguzi na wakunga ni sehemu ya kundi kubwa la watoa huduma za Afya, kwa takribani asilimia 60 hadi 80 ambapo wanatakiwa kutoa huduma kwa kuzingatia Maadili, Sheria, kanuni na taratibu ili kuhakikisha jamii inapata huduma bora na Salama.

Baraza la uuguzi na ukunga Tanzania lipo mkoani pwani kwa siku saba likitajia kuwafikia wauguzi na wakunga wa mkoa huo kwa ajili ya mafunzo ya sheria na maadili kwa wataaluma hao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *