THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

“Hakuna mtu anayeweza kuacha kitanda nyumbani aseme mimi nataka nikalale Hospitalini, hivi kweli unaacha kitanda chako cha tano kwa sita, ukalale Hospitali?  Kwa hiyo mara nyingi nasema hii kazi yetu ni ya ubinadamu kwa sababu ni lazima uvae viatu vya mgonjwa na hakuna nayejua yatakayompata dakika mbili kuanzia sasa, unaweza kushitukia na wewe umelazwa na watoa huduma si ni sisi wenyewe, hivi unafikiri tutabadilisha tabia za kutelekeza wagojwa kama tumezoea kutelekeza   tuseme Agness Mtawa, naumwa tumuhudumie vizuri”

Kauli hiyo imetolewa na Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga chini Bi. Agness Mtawa, wakati akiwafundisha Wauguzi na Wakunga wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani, Novemba 13/2023, kuhusu maadili ya taaluma za Uuguzi na Ukunga ikiwa ni muendelezo wa kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta hizo mbili.

Akizungumzia umuhimu wa kuzingatia maadili amewataka wauguzi na wakunga kuzingatia maadili ya taaluma yao, ikiwa ni pamoja na usiri wa taarifa za mgonjwa, kuweka kumbukumbu za wagonjwa, kumshirikisha mgojwa kwa kufafanua aina ya matibabu anayopewa ikiwa ni pamoja na kutomtelekeza mgonjwa.

Naye Mwanasheria wa Baraza Wakili George Shilla, amewataka Wauguzi na Wakunga Nchini kuhakikisha kila mwanataaluma anakuwa na leseni kabla ya kuanza kutekeleza majukumu ya kitaaluma pamoja na kuwakumbusha Wauguzi na Wakunga waliopo kazini umuhimu wa kuhuisha leseni zao kwa wakati.

Ikumbukwe kuwa,Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania lilianzishwa mwaka 1953 chini ya sheria ya Wauguzi na Wakunga kwa shabaha ya kusimamia taaluma za Uuguzi na Ukunga ili kuhakikisha jamii inapata huduma iliyosalama huku muuguzi au mkunga anayetoa huduma hapa Nchini lazima awe na leseni ya Baraza, baada ya kuridhika kuwa amefikia viwango vya kitaluuma vinavyokubalika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *