THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Maofisa wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) Ndimmyake Mwakapiso na Ezekiel Nyalusi, wameanza ziara ya siku saba ya kuzuru vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam.

Katika siku ya kwanza leo Disemba 11/2023, kitengo kimefanya ziara katika chumba cha uchakataji wa Habari za Gazeti hilo mashuhuri Nchini.

Wakiongozwa mwenyeji wao ambaye pia ni Mhariri Mkongwe na mwenye uzeefu wa zaidi ya miaka 20 Rashid Kenjo, Maafisa hao kutoka (TNMC), wamejifunza utendaji kazi wa kilasiku wa chombo hicho na kisha kupitishwa na kupata maelezo ya idara mbalimbali ikiwa ni pamoja na Idara ya habari Mtandao, (Online Media), Kitengo cha Mikakati, Idara ya Magazeti ya Kingereza, Kitengo cha Uhusiano kwa Umma, Idara ya Masoko na mauzo pamoja na kufanya mazungumzo na timu ya Wahariri.

Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano cha Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) kinafanya ziara hii ya kitaaluma kwenye vyombo vya habari Jijini Dar es Salaamu kwa lengo la kuitangaza Taasisi, kujenga uhusiano na vyombo vya Habari lakini pia kubadilishana uzoefu na umahiri katika suala la kuhabarisha kwa njia ya Mtandao (Online Media)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *