THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania limepeleka misaada ya kibinadamu katika wilaya ya Hanang palipokumbwa na Maafa ya maporomoko ya tope, Desemba 3 mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 89, majeruhi na wengine wakikosa makazi.

Akikabidhi Misaada hiyo Bw. Augustino Mwita ambaye ni Mkaguzi wa ndani wa Baraza la Uuguzi na Ukunga, amesema watumishi wa Baraza wameguswa na tukio hilo na kuamua kujichanga kutoa faraja kwa waathiriwa kwa kutoa mavazi na vifaa vingine.

Mkuu wa kitengo cha Huduma za Sheria Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania George Shilla ametoa pole kwa Rais Samia Suluhu Hassan na wana Hanang’ wote kwa janga lililowapata.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Hanang’ Janeth Mayanja ameshukuru kwa msaada huo akiwataka wengine waendelee kujitolea haswa vifaa vya ujenzi ili wasio na makazi waweze kujengewa nyumba.

Hata hivyo serikali na wadau mbalimbali wameendelea kujitokeza na kujitolea misaada mbalimbali ya kibinadamu kwa wahanga hao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *