THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Ofisi ya Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania inawatangazia   watahiniwa wote kufika vituo vya Mtihani wa usajili na leseni siku ya tarehe 28.12.2023 saa mbili asubuhi kwa ajili ya maelekezo.

Aidha, kadi za indexin vitatolewa siku hiyo kwa ambao hawakuchukua awali, lakini pia namba za Mtihani zitabandikwa kwenye mbao za matangazo zilizopo kituoni hapo na wale ambao hawakukamilisha taratibu za maombi, hawataruhusiwa kuingia kwenye chumba cha Mtihani siku ya Mtihani yaani tarehe 29.12.2023.

Aidha, watahiniwa wote wanatakiwa kufika kituo cha Mtihani saa moja kamili 01:00 Asubuhi wakiwa wamevaa mavazi nadhifu kwa mujibu wa muongozo wa mavazi kwa watumishi wa umma pia wanatakiwa kuja na vifaa vifuatavyo kwa ajili ya Mtihani; Picha moja (passport size) zenye viwango vilivyoelekezwa, kalamu nyeusi au penseli aina ya HB, ufutio. na kitambulisho kwa watahiniwa wa ngazi ya Shahada na wanaorudia Mtihani. Aidha, kwa watahiniwa wanaofanya kwa mara ya kwanza kwa ngazi ya Stashahada na Astashahada waje na kadi ya Indexin.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *