THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Timu ya Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania imetoa Mafunzo ya Maadili na Sheria kwa Wauguzi na Wakunga 212 katika Halmashauri ya Mji Ifakara,Kituo cha Afya Kibaoni,Hospitali ya St Fransis,Hospitali ya Kilombero,Wauguzi kutoka Hamashauri Wilaya Mlimba na Chuo cha Uuguzi na Ukunga Edgar Maranta Mkoani Morogoro.

Ikumbukwe kuwa, Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania ni chombo cha Kisheria kilichoanzishwa chini ya Sheria ya Uuguzi na Ukunga ya 2010, na Kanuni zake kwa ajili ya kutoa, kulinda, kuimarisha, na kuhifadhi Afya ya Jamii, Usalama na Ustawi kupitia usimamizi na Udhibiti wa Shughuli za Mafunzo ya Uuguzi na Ukunga na utoaji wao wa huduma.

Kwa mujibu wa Sheria hii Baraza lina wajibu wa kuanzisha na kuhakiki viwango vya utendaji, ufanyaji kazi na Maadili yanayotarajiwa kutoka kwa wauguzi na wakunga.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *