THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) Bi. Agnesi Mtawa, leo amefanya mahojiano na shirika la Utangazaji Tanzania TBC Kupitia kipindi cha Asubuhi kinachofamika kwa jina la Jambo Tanzania.

Akizungumza katika mahojiano hayo maalum yenye lengo la kuangazia mafanikio ya Baraza kuelekea maadhimisho ya miaka 71 tangu kuanzishwa mwaka 1953, Msajili ametaja baadhi ya mafanikio makubwa yaliyofikiwa ikiwa ni pamoja na; Kukua kwa Baraza na kufikia hadhi ya Taasisi ya Serikali nyenye Muundo wake wa kiutumishi ukiainisha kurugenzi, Sehemu na Vitengo vya Taasisi.

Kuongezeka kwa idadi ya wanataaluma wa kada ya Uuguzi na Ukunga kutoka watumishi wachache mwaka 1953 mpaka watumishi 52,000 mwaka 2024, ambao wamegawanyika katika ngazi za Elimu kuanzia Astashahada mpaka Shahada ya uzamivu (Phd) na kundi kubwa ni ngazi ya Stashahada ambao ni 26, 450.

Kuanzishwa kwa mfumo wa kielekitronoki wa kutunza orodha na taarifa za wauguzi na wakunga kote nchini, ambapo hapo awali orodha ilikuwa inatunzwa kwenye daftari la nakala ngumu ambalo lilifahamika kama Kalamazoo.

Baraza la Uuguzi na Ukunga linatarajia kutimiza miaka 71 ifikapo Jummanne ya tarehe 19/03/2024

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *