THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

“Ilituweze kuboresha huduma ya jamii inatakiwa kuwa na wauguzi wenye sifa ya kuhudumia jamii, “ni kweli tukubali kuwa tupo na shida ya walimu wasio na sifa ya kufundisha wanafunzi haiwezekani mwalimu umetoka chuo ukaenda kufundisha wanafunzi wakati hujawahi kufanya kazi kwa vitendo” Bi. Ziada.

Bi.ziada ameongeza kuwa kuna umuhim mkubwa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania kukaa pamoja na NaCTE na wadau wengine wa elimu ya kuona namna bora ya kuweka utaratibu mzuri wa utoaji mafunzo ya kada ya Uuguzi na Ukunga Tanzania.

Muuguzi mkuu wa serikali Bi.Ziada Sellah ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa mwaka wa wauguzi viongozi wa Mikoa, Halmashauri, Hospitali ya Taifa, Hospitali za Kanda, Hospitali za Rufaa za Mikoa, Hospitali maalum, wauguzi wakufunzi kutoka Vyuo vikuu na Vyuo vya kati ulioandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Lengo la Mkutano huu ni kuwaleta pamoja Wauguzi viongozi kutoka ngazi zote za kutolea huduma za Afya chini na wadau mbalimbali wa Afya kujadili na kupanga mikakati ya pamoja ya namna bora ya kuondoa malalamiko kwa wananchi kwa kuhakikisha huduma zinazojali utu, heshima, upendo na mawasiliano madhubuti baina ya mtoa huduma na mteja zinatolewa, pia kuweka mikakati ya kuimarisha usimamizi wa wanafunzi wauguzi katika maeneo ya kutolea huduma za afya.

Mkutano huu unafanyika Jijini Dodoma kuanzia tarehe 18/03/2024 hadi 20/03/2024 Umebebwa na Kauli mbiu “Huduma sitaha na mawasiliano Madhubuti ni wajibu wa kila mtoa huduma za Afya”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *