THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Baraza la uuguzi na ukunga Tanzania TNMC, limeendelea kukusanya maoni kwa wauguzi na wakunga wa Halmashauri za Wilaya za Wanging”ombe na Makete mkoani Jombe, zoezi hili linalengo la kuihuisha ili kuiboresha Sheria ya uuguzi na ukunga ya Mwaka 2010.

Wakizungumza katika vikao maalumu vya kukusanya maoni hayo, wanataaluma hao wametoa maoni ya kuboresha Sheria hiyo katika vipengele mbalimbali ikiwa ni pamoja na uendeshaji wa vituo binafsi vya kutolea huduma za uuguzi na ukunga, makosa ya kitaaluma na athabu zake pamoja na Suala la leseni kwa wanataaluma wa kada hiyo.

Sheria inayosimamia taaluma na wanataaluma wa kada za uuguzi na ukunga ilitungwa kwa mara ya kwanza mwaka 1952 kabla ya kuhuishwa mwaka 1997 na kisha kutungwa mpya mwaka 2010 ambapo maoni yanayotolewa yanalengo la kuihuisha ili iendane na wakati uliopo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *