Kikosi cha Maafisa kutoka Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) kipo mkoani Tanga kwaajili ya kuhamasisha Maadili, Sheria ya Uuguzi na Ukunga na huduma bora kwa wateja.
Pamoja na shughuli hizo watatembelea vyuo vya Uuguzi na Ukunga ili kujionea hali halisi ya utoaji wa Mafunzo hayo ikiwa ni pamoja na kusisitiza uzingatiaji wa miongozo.