Viongozi wa Chama cha “wanafiziotherapi” Tanzania (Association of Physiotherapists in Tanzania) leo oktoba 10,2024 wameitembelea ofisi ya Msajili wa Baraza la Uuguzi na Uunga Tanzania kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali ya utendaji kazi wa TNMC.
Pamoja na mambo mengine mengi Viongozi hao ndg. Jerusalem Makotore(kulia) ambaye ni Mhazini na Dietrich Chussi(kushoto) ambaye ni katibu wameonesha kufurahia mapokezi hayo waliyoyapata kutoka ofisi ya Msajili.
Kaimu Msajili Bi. Jane Mazigo amewapongeza wataalam hao kwa kutembelea Ofisi ya Msajili na kuwaeleza namna Baraza linavyosimamia taaluma na kuhakikisha jamii inapata huduma bora aidha, amewakaribisha kwa wakati mwingine watakapohitaji kujifunza zaidi.
Ikumbukwe kuwa, Baraza la Uuguzi na Ukunga ni Mamlaka ya Kisheria inayosimamia wanataaluma na Taaluma za Uuguzi na Ukunga Tanzania, chini ya Sheria ya Mwaka 2010 (The Nursing and Midwifery Act, 2010) ili kuhakikisha huduma zinazotolewa na Wauguzi na Wakunga nchini Tanzania ni za kiwango kinachokubalika na salama kwa jamii.