THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Madaktari Wasio na Mipaka (MEDECINS SANS FRONTIERES- MSF) wametembelea ofisi ya msajili kufahamu utendaji kazi wake hususaji kuhusu sajili za wauguzi na wakunga hapa nchini wakiwa kama wadau katika utoaji wa huduma za kiafya hapa nchini.

Madaktari Wasio na Mipaka (MEDECINS SANS FRONTIERES- MSF) ni akika nani?

Hili ni Shirika lisilo la kiserikali na la kimataifa linaoundwa na Madaktari na wafanyakazi wa sekta ya Afya.

Pia linapokea wafanyakazi kutoka kwenye taaluma zingine ikiwemo wauguzi na wakunga ambao wanaweza kusaidia kutimiza malengo ya shirika. Wafanyakazi wake wote wanakubali kuheshimu sheria na kanuni:

MSF inatoa msaada kwa watu walio kwenye shida, walioathirika na majanga ya asili au ya kibinadamu na waathirika wa vita. Na wanafanya hivyo bila ya ubaguzi wa rangi,dini au misimamo ya kisiasa MSF inafanya kazi bila kuegemea upande wowote kwa mujibu wa maadili ya kitabibu na haki ya msaada wa kibinadamu, shirika hili lina uhuru wa kutosha katika kufanya kazi zake.

Hata hivyo, Wafanyakazi wa MSF wanatakiwa kuheshimu maadili ya kitaaluma na kulinda uhuru wake dhidi ya ushawishi wa kisiasa, kidini na kiuchumi. Wafanyakazi wanazoweza kukabiliana nazo wawapo kwenye kazi zao na hawapaswi kuomba malipo yoyote ya fidia zaidi ya yale ambayo MSF inaweza kuwalipa.