THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Mwenyekiti wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania Prof.Lilian Mselle, ameongoza kikao cha Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania kinachofanyika Ukumbi mdogo wa Mikutano wa Jakaya Kikwete.

Kikao hicho cha uendeshaji wa mashitaka huketi na kutolewa maamuzi kwa mujibu wa Sheria ya uuguzi na ukunga.

Aidha, kwamujibu wa Sheria hiyo 31(1) Mtu yeyote ambaye hajaridhika na uamuzi wa Baraza anaweza, ndani ya miezi mitatu toka tarehe ya kupata taarifa ya uamuzi, kukata rufaa kwa Waziri.

(2) Waziri anaweza kutupilia mbali au kuruhusu rufaa yoyote au kubadili au kutofautiana na uamuzi wa Baraza au kutoa amri yoyote atakayoona inafaa.

Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania ni Mamlaka ya Kisheria iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Uuguzi na Ukunga ya 2010, na Kanuni zake kwa lengo la kuhakikisha huduma zitolewazo na wauguzi na wakunga zinaubora na salama kwa wateja.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *