THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA NURSING AND MIDWIFERY COUNCIL

Search

Dodoma-Tanzania 09.01.2024.

Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania anawaarifu Wahitimu wote wa Kozi za Uuguzi na Ukunga waliofaulu Mtihani wa Usajili na Leseni uliofanyika tarehe 07/9/2023, Kuwa Mahafali ya kutoa Vyeti vya Usajili na Leseni yatafanyika siku ya Jumanne tarehe 16/1/2024 kuanzia Saa1:00 Asubuhi katika Ukumbi wa “CATHEDRAL SOCIAL HALLJijini-Dodoma

Maelekezo ya kufika Ukumbini,Ukumbi upo HAZINA, Mkabala na Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki-Dodoma, barabara inayotokea usawa wa geti la bima Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Dodoma kuelekea lango kuu la Hospitali ya Taifa ya Afya ya akili Mirembe.

Washiriki wote mnatakiwa kuthibitisha Ushiriki wenu kwa kujaza fomu ya Mahafali kupitia Tovuti ya Baraza la Uuguzi na Ukunga www.tnmc.go.tz.

Hivyo, washiriki wote wa mahafali watatakiwa kuvaa Sare ya Kitaaluma “Professional Uniform iliyoidhinishwa na Baraza la Uuguzi na Ukunga kama ifuatavyo: –

  1. WANAWAKE- Magauni au Suruali na Blauzi rangi nyeupe ndefu.
  2. WANAUME- Kaunda suti- Shati jeupe na Suruali dark blue
  3. VIATU– Vinavyofunika miguu na siyo vya wazi, viwe vya rangi nyeusi, nyeupe au brown.
  4. Kitambulisho chochote chenye picha ya mhusika  kinachomtambulisha

Aidha, Katika Mahali haya Mada mbalimbali zitatolewa kisha Kiapo.

NB: Sandozi au Kandambili haviruhusiwi. Kwa Mawasiliano zaidi piga namba 0655035078 na 0762003800

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *