Author: super-admin

  • HAWA HAPA WAJUMBE WA BARAZA LA UUGUZI NA UKUNGA TANZANIA (TNMC)

    HAWA HAPA WAJUMBE WA BARAZA LA UUGUZI NA UKUNGA TANZANIA (TNMC)

    Waziri wa Afya Mhe. Jenesta Mhagama (Mbunge) amefanya uteuzi na kuzindua Baraza jipya la Uuguzi na Ukunga Tanzania(TNMC) lenye jumla ya   wa wajumbe 12 baada ya wajumbe wa Baraza la awali kumaliza muda wao

    Uteuzi wa wajumbe 12 wa Baraza ni kwa Mujibu wa kifunga namba 5 – (1) cha Sheria ya Uuguzi na Ukunga ya mwaka 2010 ambacho kimempa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya Afya kufanya uteuzi wa wajumbe wa Baraza.

    Aidha, wajumbe wateule watahudumu kwa kipindi kisichozidi miaka mitatu tangu kuteuliwa kwao.

    Wajumbe hao ni Pamoja na;

    1.Prof.Lilian Mselle,- Mwenyekiti ambaye ni Muuguzi mwandamizi,na na Mhadhili kutoka Chuo Kikuu cha Muhimbili, Shule ya Uuguzi.

    (2). Dkt. Bankanie Vicent, Mjumbe anawakilisha waalimu wauguzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma

    (3) Bw. Alexander Baluhya Mjumbe-anayewakilisha Chama cha wauguzi Tanzania, kutoka Chuo cha Afya na Sayansi shirikishi Kabanga (4) Bi. Hilda Ndambalilo Mjumbe- Anawakilisha wauguzi wakuu wa mikoa ni muuguzi mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,

    (5) Bi. Brenda Kitali Mjumbe- anawakilisha Wauguzi wakuu kutoka Hospitali za Rufaa, anatoka Hospitali ya KCMC,

    (6) Bw. Sulle Samwel, Mjumbe- anawakilisha wauguzi kutoka Hospitali binafsi, anatoka Hospitali ya Haydom Manyara.

    Wajumbe wengine ni; (7) Bi.Tumaini Lawrence, mjumbe- kutoka kwenye jamii anatoka Tanzania Association of Women Certified Accounts, (8) Bi. Ziada Sellah, mjumbe-Muuguzi mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Tanzania, anatoka Wizara ya Afya Dodoma (9)

    Bi. Ruhama Masanika, mjumbe-anawakilisha wauguzi ngazi ya cheti(EN) kutoka Hospitali ya Mkoa wa Dodoma,

    (10) Wakili Bavoo Junus, mjumbe kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,

    (11) Dkt. Alfred Sabahene, mjumbe- Kutoka kwenye jamii, kutoka Chuo Kikuu cha ST John Dodoma na

    (12) Dkt. Fabian Byesigwa mjumbe- Anawakilisha taaluma nyingine,ni kutoka ofisi ya RMO  Mkoa wa mara.

    Mh.Waziri amezindua baraza jipya na kuwapa wajumbe nyenzo za utekelezaji majukumu yao ambazo ni Sheria ya Uuguzi na Ukunga ya Mwaka 2010 na Kanuni zake Pamoja na miongozo mingine.

    Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania TMNC ni mamlaka ya kisheria inayosimamia wanataaluma na taaluma za uuguzi na ukunga Tanzania, Chini ya Sheria ya Uuguzi na ukunga ya mwaka 2010 na kanuni zake (The Nursing and Midwifery Act 2010) ili kuhakikisha kuwa huduma zinazotolewa na wauguzi na wakunga nchini zinakiwango kinachokubalika na salama kwa jamii.

  • WAZIRI WA AFYA ATEUA NA KUZINDUA BARAZA LA TNMC LEO

    WAZIRI WA AFYA ATEUA NA KUZINDUA BARAZA LA TNMC LEO

    Waziri wa Afya Mhe. Jenesta Mhagama (Mbunge) amefanya uteuzi na kuzindua Baraza jipya la Uuguzi na Ukunga Tanzania(TNMC) lenye jumla ya wajumbe 12 baada ya wajumbe wa Baraza la awali kumaliza muda wao.

    Uteuzi wa wajumbe 12 wa Baraza ni kwa Mujibu wa kifunga namba 5 – (1) cha Sheria iliyotungwa na Bunge ya Uuguzi na Ukunga ya mwaka 2010 ambacho kimempa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya Afya kufanya uteuzi wa wajumbe wa Baraza.

    Akizungumzana katika hafla ya uzinduzi amewataka wajumbe hao kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Baraza kuhakikisha wanasimamia, wajibu, weledi na kudhibiti wanotaka kuvunja Sheria, kanuni na taratibu za sekta ya Afya kupitia taaluma ya Uuguzi na Ukunga.

    Kama serikali hatutamani kusikia muuguzi au Mkunga amavunja taratibu katika kutekeleza majukumu yake kwa sababu huyo mmoja anaharibu image ya wauguzi na wakunga wote, kwa hiyo mmepewa heshima ili ninyi mtusaidie na pale mtakapotakiwa kufanya dhidi ya wale wanaoharibu heshima na sifa ya taaluma yetu, muongozwe na uzalendo kwa maslahi ya jamii nzima ya Watanzania.
    wajumbe wapya watahudumu kwa kipindi kisichozidi miaka mitatu tangu kuteuliwa kwao.

    Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania TMNC ni mamlaka ya kisheria inayosimamia wanataaluma na taaluma za uuguzi na ukunga Tanzania, Chini ya Sheria ya Uuguzi na ukunga ya mwaka 2010 na kanuni zake (The Nursing and Midwifery Act 2010) ili kuhakikisha kuwa huduma zinazotolewa na wauguzi na wakunga nchini zinakiwango kinachokubalika na salama kwa jamii.

  • WATAHINIWA 5147 KUFANYA MTIHANI WA USAJILI NA LESENI

    WATAHINIWA 5147 KUFANYA MTIHANI WA USAJILI NA LESENI

    Jumla ya watahiniwa 5147 waliohitimu katika vyuo mbalimbali, wanatarajiwa kufanya Mtihani wa usajili na leseni unaoratibiwa na Baraza la uuguzi na ukunga Tanzania (TNMC) katika vituo vilivyotengwa kwenye mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam, Iringa, Tabora, Mwanza na Arusha.

    Hilo limebainishwa na Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa, mjini Kibaha mkoani Pwani, alipokutana na waandishi wa habari.

    Usajili amesema mtihani huo utafanyika Ijumaa ya Disemba 20, 2024, ambapo kati ya watahiniwa 5147, wanajumuisha wahitimu ngazi ya Astashahada 86, Stashahada 4498, Shahada ya Uuguzi 537, Shahada ya Ukunga 11 na Shahada ya Uuguzi katika Utaoji dawa za usingizi na ganzi 11.

    Aidha, Bi. Mtawa ameongeza kwa kuwataka watahiniwa wa Mtihani wa kada za Uuguzi na Ukunga, Kujiepusha na vitendo vya udanyanyifu wakati wa kufanya mtihani kwani atakayebainika kufanya hivyo atakabiliwa na adhabu ya kufutiwa matokeo ya Mtihani huo.

  • WAUGUZI NA WAKUNGA ZAIDI YA 1200 WATUNUKIWA  VYETI NA LESENI ZA KITAALUMA.

    WAUGUZI NA WAKUNGA ZAIDI YA 1200 WATUNUKIWA VYETI NA LESENI ZA KITAALUMA.

    Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) limewatunuku wauguzi na wakunga 1222 Leseni na  vyeti vya kitaaluma hii leo 13.12.2024 katika Mahafali ya 12 ya kitaaluma yaliyofanyika katika ukumbi wa st.peter’s swaswa uliopo Jijini Dodoma.

    Akihutubia katika hafla ya kitaaluma Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na ukunga nchini na Muuguzi Mkuu wa Serikali Bi.Ziada sellah amewataka wauguzi na wakunga hao kuzingatia maadili ya Uuguzi na Ukunga hapa nchini kwa kufuata miongozo ya kitaaluma.

    “sasa leo mmeshatunukiwa vyeti na leseni hatutegemei muuguzi na mkunga kufanya mambo kinyume na miongozo ya kitaaluma mkaihudumie jamii kwa kutoa huduma zenye utu na staha” alisema Bi. Ziada

    Katika hatua nyingine Muuguzi Mkuu wa serikali amesisitiza umuhimu wa  wataaluma hao kujiendeleza kitaaluma kwani taaluma ya Uuguzi na Ukunga inakuwa kila uchwao.

    Naye Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga  Bi. Agnes Mtawa amesisitiza kwa wauguzi na wakunga kufanya kazi kwa kuzingatia mawanda yao ya kazi, huku akisisitiza kuwa na lugha nzuri wakati wa utoaji huduma za Uuguzi na Ukunga.

    “sasa isiwe unafika kwa mgonjwa amelala wewe unamchoma sindano akishituka unamwambia  tulia… ulikuwa hujui ni mud awa sindano? Mimi nasema ni vizuri kuwa na lugha nzuri na wateja wetu wakati wa utoaji huduma.” Alisema Bi.Mtawa

    Kwa Upande wake Mkurugenzi wa usajili,leseni na Maadili Bi.Jane Mazigo Pamoja na kusisitiza misingi ya maadili kwa wataaluma amewataka wauguzi na wakunga kutumia muda wao mwingi kujifunza ili kuwa wabobezi katika taaluma ya Uuguzi na Ukunga.

  • WATOA HUDUMA CHUMBA CHA UPASUAJI MTWARA-SZRH WANUFAIKA NA MAFUNZO KUTOKA TNMC.

    WATOA HUDUMA CHUMBA CHA UPASUAJI MTWARA-SZRH WANUFAIKA NA MAFUNZO KUTOKA TNMC.

    Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC), limetoa mafunzo elekezi kwa Madaktari, wauguzi,wakunga na wauguzi wataalamu wa dawa za usingizi na ganzi wanaofanya kazi katika vyumba vya upasuaji pamoja na baadhi ya watumishi kutoka vitengo mbalimbali vya kutolea huduma wapatao 45 katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini, juu ya namna bora ya kutoa huduma katika chumba cha Upasuaji “Theatre Management” kwa lengo la kumlinda mgonjwa kuwa salama baada ya upasuaji.

    Mafunzo yanayodumu kwa muda wa siku 14 yanaongozwa na Afisa Muuguzi Mbobezi kutoka Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania Bi. Salome Kassanga akisaidiana na Muuguzi mbobezi katika chumba cha upasuaji Bi Happiness Liya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa – Ligula.

    Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mwezeshaji kutoka Baraza la Uuguzi na Ukunga amesema kuwa, lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Madaktari, Wauguzi, Wakunga na Wataalamu wengine katika chumba cha Upasuaji ili kuboresha huduma kwenye chumba cha Upasuaji na kukidhi viwango vya Kimataifa. “Tunatoa mafunzo haya ili kuhakikisha kuwa vyumba vya upasuaji kunakuwa na misingi bora ya usimamiaji na uendeshaji, misingi ya kudhibiti maambukizi kwa wagonjwa (IPC), uzingatiaji wa Maadili, Sheria, kanuni na miongozo katika chumba cha upasuaji, uvaaji wa sare maalumu za chumba cha upasuaji kulingana na miongozo husika, uzingatiaji wa kuweka taarifa za wagonjwa wanaopatiwa huduma za upasuaji (Documentation), pamoja na kulinda usalama wa mgonjwa na watoa huduma” alisema Bi. Kassanga.

    Hata hivyo, Bi. Kassanga ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha watumishi juu ya utoaji wa huduma kwa kuzingatia Maadili, Miiko, Uadilifu, ikiwa ni Pamoja na uvaaji wa Sare maalumu za chumba cha upasuaji kulingana na miongozo husika, uzingatiaji wa kuweka taarifa sahihi za wateja wanaopatiwa huduma (Documentation), pamoja na kulinda usalama wa mgonjwa na watoa huduma” alisema Bi. Kassanga.